Diamond Aweka Wazi Mahusiano Yake na Baba Yake Mzazi

Diamond Aweka Wazi Mahusiano Yake na Baba Yake Mzazi
Baada ya tetesi za muda mrefu kuzagaa kuwa Msanii wa Muziki nchini Tanzania, Diamond Platnumz kuwa hana mahusiano mazuri na baba yake mzazi, Hatimaye Diamond ameweka wazi ukweli wote kwa kukanusha taarifa hizo.

Diamond amesema kuna watu wenye hira ndio wanaokuza mambo lakini yeye huwa anawasiliana naye na huwa anamsaidia pale anapokuwa na kitu.

Ingawaje Diamond amekiri wazi kwamba hana mazoea naye kama ilivyo kwa mama yake mzazi lakini hakuna bifu kama baadhi ya watu wanavyokuza mambo.

Kwa upande mwingine, Diamond amewakanya baadhi ya watu ambao wanampeleka baba yake hadi kwenye geti lake na kumpiga picha ili kuupotosha umma kuwa amemfungia geti baba yake, waache hiyo tabia kwa sababu inaathiri hadi familia nyingine.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad