Kamanda Msangi Afunguka Kuhusu Tukio la Ndugu Waliofukua Mwili wa Marehemu

Kamanda Msangi Afunguka Kuhusu Tukio la Ndugu Waliofukua Mwili wa Marehemu
Kamanda wa Polisi wa Mwanza Ahmed Msangi leo February 22, 2018 ametolea ufafanuzi wa tukio la kufukua mwili wa marehemu ili ndugu wajiridhishe baada ya kuwa na hofu na kifo cha ndugu yao aliyefariki akiwa anafanyiwa upasuaji katika kituo cha Afya cha Filoleli Mwanza.

Kamanda Msangi ameeleza kuwa marehemu Ashura Shaban Salum, 40, kabla ya kifo chake alifanyiwa upasuaji na baadaye kupoteza maisha na mwili wake ulipelekwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti, madaktari ilibidi wauchome mwili sindano ili usiharibike.

Kwenye mchakato huo wa kumchoma sindano, ilibidi madaktari wachane eneo la paja ili kupata mshipa huo wa kuchoma sindano jambo ambalo ndilo ndugu walilalamikia baada ya kukuta jeraha hilo kwenye paja la ndugu yao, wakihisi pengine kuna viungo vingine vya mwili vimetolewa.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad