Kikwete Amlilia Kingunge "Maneno ya Kutosha Kubeba Uzito wa Simanzi Zake"

Kikwete Amlilia Kingunge "Maneno ya Kutosha Kubeba Uzito wa Simanzi Zake"
Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa hana maneno ya kutosha kubeba uzito wa simanzi zake kwa Mwanasiasa Mkongwe Kingunge Ngombali Mwiru.

Dkt Kikwete ameeleza kuwa Mzee Kingunge ni moja ya walezi wake waliomlea kisiasa na wametoka mbali.

“Nimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za kifo cha Mzee Kingunge Ngombare Mwiru.Sina maneno ya kutosha kubeba uzito wa simanzi zangu.Mzee huyu ni moja ya walezi wangu kisiasa. Tumetoka nae mbali. Natoa pole zangu kwa familia na Watanzania wote. Alale kwa amani,“ ameandika Dkt. Kikwete katika ukurasa wake wa Twitter.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad