Maneno ya Ridhiwani Kufuatiwa Kifo cha Kingunge “Nimeamka Katika Usingizi, Najiuliza Niandike?”

Maneno ya Ridhiwani Kufuatiwa Kifo cha Kingunge “Nimeamka Katika Usingizi, Najiuliza Niandike?”
Bado watanzania na wanasiasa mbalimbali wapo katika majonzi na maombolezo ya kifo cha mwanasiasa mkongwe ambaye pia amewahi kuwa kiongozi wa serikali Kingunge Ngombale Mwiru ambaye atazikwa leo February 5 2018.

Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete ni moja kati ya wanasiasa waliyoguswa na msiba wa mzee Kingunge na ameamua kutumia ukurasa wake wa instagram kuandika ujumbe huu.

“Nimeamka katika Usingizi nimemkumbuka Mzee Kingunge. Kwangu mimi huyu Mwalimu wa Itikadi ya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea atabaki kuwa Mwalimu. Najiuliza niandike au niache yabaki kifuani kwangu”

“Iko upande wa nafsi yangu unaniambia niandike kwa yale ninayofahamu kuhusiana na mzee kingunge na huko nafasi unaniambia nisubiri tukuhifadhi kwa nyumba ya milele ili niandike”

“Nitaandika tu……Ulikuwa Mzazi, Mlezi, mtuliza maumivu,rafiki , mcheshi na Uliyeamini katika kile unachokiamini.haukukamilika kama walivyokuwa wengine. ……Nitaandika Ngoja Tukuhifadhi Coming Soon…..Nitaandika”
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad