Martini Kadinda Afunguka Kuhusu Ukaribu Wake na Wema Swpetu

Martini Kadinda Afunguka Kuhusu Ukaribu Wake na Wema Swpetu
Aliyekuwa meneja wa Wema Sepetu Martin Kadinda amefunguka ni kwanini kipindi hiki haonekani karibu sana na mrembo huyo kama ilivyokuwa awali.

Mbunifu huyo wa mavazi amesema si kwamba hayupo karibu na Wema ila kazi wanazofanya kwa sasa hazihitaji kusikika katika vyombo vya habari.

“Kuna wakati unafika inabidi ufanye vitu vingine sio kwamba sipo karibu naye lakini tume-focus kwenye vitu vingine zaidi ambavyo we think sio media inahitajika kuvijua sana but kidogo ambacho wanakipata ndio wanatakiwa kukipata,” amesema.

Marthin ameongeza kuwa Wema alikuwa anachukulia kawaida mambo yake ambayo hata yasingetakiwa kusikika katika vyombo vya habari lakini wamemueleza hilo halifai kwani vitu vingi havifanikiwa vikiwa kwenye media kila siku.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad