Mchezaji wa Azam Augua Ghafla Atolewa Kwenye Kikosi

Klabu ya Mabingwa Afrika Mashariki na Kati, Azam FC imemuondoa mchezaji wake Yahya Zayd kwenye kikosi kinachotarajiwa kucheza leo dhidi ya Kagera Sugar FC baada ya kuugua ghafla mchana huu.

Hayo yamebainishwa na taarifa iliyotolewa na klabu hiyo na kusema nafasi yake itachukuliwa na mshambuliaji Mbaraka Yusuph ambaye alipaswa kuanzia kutokea benchi.

Mechi hiyo ya Azam FC ni muendelezo wa michuano ya VPL mzunguko wa 18 ambao utapigwa katika dimba la Kaitaba mkoani Kagera.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad