Mnyama ‘Simba SC’ Hakamatiki, Maafande wa Ruvu Shooting watafunwa

Klabu ya Simba imeendeleza ubabe kwenye mzunguuko wa pili wa Ligi Kuu Vodacom Tanzania Bara kwa kwa ushindi mnene wa goli 3-0 dhidi ya Maafande wa ‘Ruvu Shooting’.

Magoli ya Simba yamefungwa na Nahodha wa timu hiyo, John Bocco magoli mawili huku goli la tatu likifungwa na Mzamiru Yassin.

Kwa ushindi huo Simba inajidhatiti kileleni kwa alama 38 ikifuatiwa na klabu ya Azam FC alama 33, Mahasimu wao Yanga wakisalia nafasi ya tatu na alama 31.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad