Niki wa Pili Awafunda Wanandoa "Vyombo Hata Vikiwa Vichafu Namna Gani Huwezi Kwenda Vioshea Lalalani"

Niki wa Pili Awafunda Wanandoa "Vyombo Hata Vikiwa Vichafu Namna Nani Huwezi Kwenda Vioshea Lalalani"
Msanii kutoka kampuni ya Weusi, Nikki wa Pili amefunguka na kuitaka jamii hasa watu waliopo kwenye ndoa kuacha tabia ya kusuluhisha matatizo yao kupita majirani na badala amewashauri wafanyie chumbani.


Nikki ameeleza hayo kupitia ukurasa wake maalumu wa kijamii baada ya kuwepo rundo la kesi za ndoa zinaanikwa kwenye mitandao ya kijamii huku wengine mtaani kwa lengo la kupata msaada juu ya tatizo hilo huku wengine wakitumia kama fimbo kuwadhalilisha wenza wao.

"Vyombo hata vikiwa vichafu namna gani huwezi kwenda vioshea jalalani, utavioshea kwenye karo tena karo safi. Basi ndoa hata kama imechafuka kiasi gani, jaribu kuisafishia chumbani sio kwa majirani au kitaani",amesema Nikki.

Nikki wa Pili ametoa ushauri huo kwa jamii ikiwa zimebakia takribani siku tano kuadhimisha siku maalumu ya wapenda nao kama wengine wanavyopenda kuita 'Valentine Day' ambapo siku hiyo inapambwa na upendo na faraja japo kuwa jamii inaimizwa kuwa na upendo kwa wenza wao siku zote.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad