Simba imerudi Anga za Kimataifa..Yamchapa Mtu 4 Bila

Simba wamerejea kwenye anga za kimataifa kwa ushindi wa magoli 4-0 dhidi ya Gendarmerie National ya Djibouti katika mchezo wa Caf Confederation Cup.

Wekundu wa Msimbazi wamesubiri kwa miaka mitano (5) mfululizo tangu waliposhiriki kwa mara ya mwisho mwaka 2012 na kuondolewa Al Ahly Shendi kwenye michuano ya vilabu bingwa Afrika.

Magoli ya Simba katika mchezo wa leo yamefungwa na Said Hamisi Ndemla, John Bocco ambaye amefunga magoli mawili huku goli la mwisho likifungwa na Emanuel Okwi.

Pacha ya ushambuliaji inayoundwa na John Bocco na Emanuel Okwi imeendeleza makali yake hadi kwenye michuano ya Afrika baada ya wawili hao kufunga magoli matatu kwa pamoja. (Bocco amefunga magoli mawili, Okwi amefunga goli moja na kumtengeneza goli moja lililofungwa na Bocco.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad