Vilio, Simanzi Vyatanda Muhimbili Wakati wa Kuchukuliwa Mwili wa Akwilina

Vilio, Simanzi Vyatanda Muhimbili Wakati wa Kuchukuliwa Mwili wa Akwilina
VILIO na simanzi vimetawala wakati wa kuchukua mwili wa aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini aliyeuawa kwa kupigwa risasi Feb 16, 2018.

Mwili wa Akwilina umechukuliwa leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kupelekwa NIT k wa ajili ya kuagwa kabla ya kupelekwa nyumbani kwao Rombo kwa mazishi.

Jeneza lenye mwili wa mwanafunzi huo liko katika gari maalumu la kubebea maiti.



Baada ya kuaga mwili wa mwanafunzi huyo, saa 10 jioni safari kuelekea wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro kwa mazishi itaanza. Akwilina atazikwa kesho.










Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad