Waliojiunganishia Bomba la Mafuta Waiomba Mahakama Iwapatie Dhamana

Waliojiunganishia Bomba la Mafuta Waiomba Mahakama Iwapatie Dhamana
Mfanyakazi Mstaafu wa Shirika la Mafuta Tanzania na Zambia (TAZAMA) Samwel Nyakirang’ani (63) na wenzake wanaokabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi wa kujiunganishia Bomba la Mafuta ya Dizeli wameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iwapatie dhamana.

Maombi hayo wameyawasilishwa kupitia Wakili wao, Kusalika Augustine mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ambapo alidai wateja wake wanahitaji kupata dhamana kwa sababu mashtaka yanayowakabili yanadhaminika.

Kutokana na maombi hayo, upande wa mashtaka uliomba kesi hiyo iahirishwe ili wajibu hoja hizo, ambapo Hakimu Simba aliahirisha kesi hiyo hadi February 22, 2018.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo  ni Nyangi Mataro ambaye ni Mwalimu wa Shule ya  msingi Ufukoni na mkazi wa Kisiwani Mkajuni Kigamboni.

Wengine ni mfanyabaishara, Farijia Ahmed, Malaki Mathia, Kristomsi Angelus, Pamfili Nkoronko na Hunry Fredrick.

Kwa pamoja washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka matatu ya uhujumu uchumi kwa kujiunganishia isivyo halali Bomba la Mafuta ya  Dizeli, kinyume cha sheria  ya Uhujumu uchumi.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad