DJ Majizzo amkumbuka Lulu kwenye siku ya wanawake Duniani


Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya EML Francis Anthony Ciza Majey (DJ Majizzo) alhamisi hii ambayo ni siku ya Wanawake Duniani, ameitumia kumkumbuka mpenzi wake, Elizabeth Michael (Lulu) ambaye amehukumiwa miaka miwili jela baada ya kukutwa na hatia ya kumuuwa bila kukusudia, mwigizaji mwenzake, Steven Kanumba.

Majizo toka hukumu hiyo isomwe alikaa kimya bila kuzungumza chochote.

Kupitia instagram, Majey ameandika ujumbe na kupost picha yake hudu akimwambia siku moja atakuja usoma ujumbe huo.

“In life all people may probably be necessary. Very useful if everything goes right or wrong. You are very important because you can be strong in all situations. Happy Women’s Day #utakujaisomaOneday,” aliandika Majey.

Pia bosi huyo ameweka profile picha ya mrembo huyo kupitia mtandao huo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad