Kajala Afunguka Kuhusu Mahusiano Yake ya Kimapenzi na Chege

Kajala Afunguka Kuhusu Mahusiano Yake ya Kimapenzi na Chege
Msanii wa filamu nchini Kajala Masanja amefunguka na kuweka wazi kuhusu tetesi zinazosambaa kuwa sasa anatoka kimapenzi na msanii wa muziki wa Bongo fleva kutoka kiumeni Chege Chigunda.


Kajala akipiga stori na Big Chawa kwenye kipindi cha Planet bongo ya East Africa Radio amekana kuhusu kutoka kimapenzi na msanii huyo na kudai kuwa hakuna jambo kama hilo na

"Mama yangu mzazi hakuna kitu kama hicho si mmeona Chege kapata mtoto juzi tu hapa, yaani mimi sina hata namba yake ya simu na haiwezi kutokea kitu kama hicho"alisisitiza Kajala

Mbali na hilo Kajala amewatakia kheri wanawake wote maarufu ambao wanakaribia kuolewa siku za karibuni na kusema kwake yeye badobado kwani anaamini mume mwema anatoka kwa Mungu hivyo atakapompata huenda na yeye ndiyo akafanya maamuzi hayo ya kuolewa sasa.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad