Kenya Yaigaragaza Tanzania Kili Marathon 2018..Haya Hapa Majina ya Washindi


Leo Jumapili Machi, 4 2018 yamefanyika mashindano ya riadha mkoani Kilimanjaro ambayo ni maarufu kwa Kili Marathon ambayo hufanyika kila mwaka.

Mashindano haya hushirikisha watu kutoka mataifa mbalimbali, ambapo wale wote ambao hufanya vizuri hupewa zawadi, wakati wengine hupewa medali ikiwa ni ishara kwa walishiriki mbio hizo.

Mashindano haya yalianza mwaka 2003 yakiwa na washiriki waliokadiriwa kuwa kati ya 300-400 lakini sasa yamekuwa yakishirikisha maelfu ya watu kutoka maeneo mbalimbali.

Katika mashindano hayo, raia kutoka Kenya wamekuwa wakifanya vizuri zaidi, na hata mwaka huu wamedhihirisha hilo baada ya kuongoza kwa kuwa na washindi wengi zaidi katika kilomita 21 na kilomita 42.

Hapa chini ni orodha ya washindi wa kilomita 21.

Geofry Torotich- Kenya
Simon Muthoni- Kenya
Shadrack Korir- Kenya
Daniel Kemoi- Kenya
Stephen Mwendwa- Kenya
Nicolas Kosgei- Kenya
Tom Mutie- Tanzania
Vincent Kimutai- Kenya
George Njoroge- Tanzania
Alex Bartilol- Kenya

Walioongoza katika kilomita 42, wote ni wawakilishi kutoka Kenya.

Cosmas Muteti- Kenya
Elkana Yego- Kenya
George Onyancha- Kenya
William Koskei- Kenya
Kipngetich Timbwol- Kenya
Francis Nzyoki- Kenya
Stephen Kimbomet- Kenya
Stephen Cimemin Njogu- Kenya
Evans Taiget- Kenya
Mark Lukuya- Kenya
Kwa mwaka 2019, mbio hizo zinatarajiwa kutimua vumbi Jumapili Machi 3, 2019.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad