Mahakamani: Shaidi Afunguka Alichokikuta Chumbani kwa Wema Baada ya Kumpekua

Mahakamani: Shaidi Afunguka Alichokikuta Chumbani kwa Wema Baada ya Kumpekua
MJUMBE wa Shina Namba 39, nyumbani anakoishi msanii wa filamu, Wema Sepetu, Steven Alphonce ambaye ni shahidi katika kesi inayomkabili staa huyo, amedai wakati wa upekuzi walikuta kipande cha sigara wala si bangi.

Alphonce amesema hayo leo Jumatatu, Machi 12, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba akiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula, wakati akitoa ushahidi wake katika kesi ya matumizi ya dawa za kulevya inayomkabili Wema na wenzake wawili na kusema alishiriki katika upekuzi nyumbani kwa Wema na kukuta kipande hicho cha sigara jikoni na chumbani kwa Wema anakohifadhi viatu na nguo.

Amedai kuwa bangi anaijua ikiwa shambani kwani aliwahi kuiona Shinyanga lakini ikiwa nje ya hapo hawezi kuitambua. Wema na wenzake wawili wanashtakiwa kwa kutumia dawa za kulevya aina ya bangi na walikamatwa Februari 4, mwaka jana.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad