Maisha Bado Ninayataka Sithubutu Kujiusisha na Unga- Davina

Maisha Bado Ninayataka Sithubutu Kujiusisha na Unga- Davina
MUIGIZAJI mahiri wa Bongo Movies, Halima Yahaya ‘Davina’ amefungukia safari zake zake za Dubai akisema ni kwa ajili ya biashara halali na si biashara haramu ya madawa ya kulevya (unga).

Akizingumza na Amani kwa njia ya simu akiwa Dubai, Davina alisema kuwa, kila anapokuwa huko kibiashara na akaweka picha mtandaoni, watu humhisihisi kuwa anasafirisha unga, jambo ambalo kamwe hawezi kulifanya.

“Yaani mimi safari zangu ni kwa ajili ya biashara zangu tu na kuhusu kujihusisha na biashara haramu za madawa ya kulevya, mimi huwa nasikia kwenye redio na kwenye magazeti, sithubutu, maisha bado ninayataka,” alisema Davina bila kutaja biashara inayompeleka Dubai mara kwa mara.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad