Manowari ya Marekani Iliyozamishwa Maka 1942 Yagunduliwa Baharini

Manowari ya Marekani Iliyozamishwa mMaka 1942 Yagunduliwa Baharini

Mabaki ya manowari ya Marekani ambayo ilizamishwa wakati wa vita vya pili vya dunia yamegunduliwa nje ya pwani ya Australia.

Manowari ya USS Lexington iligunduliwa umbali wa kilomita 3 chini ya bahari karibu kilomita 800 kutoka pwani ya Australia.

Manowari hiyo ilikuwa ilitoweka wakati wa vita vya Coral Sea, kati ya tarehe 4-8 Mei mwaka 1942. Zaidi ya wanajeshi 200 waliuawa wakati wa kuzama kwa meli hiyo.

Mabaki ya meli ya abiria iliyozamishwa 1939 yagunduliwa baharini
Jeshi la wanamaji la Marekani lilithibitisha kuwa meli hiyo ilikuwa imegunduliwa na kundi la kutafuta, linaloongozwa na mwanzilishi mwenza wa kampuni ya Microsoft Paul Allen.

Meli hiyo ilizamishwa pamoja na ndege 35 ilizokuwa imebeba
Tangazo la kugunduliwa meli hiyo na ndege 11 kati ya 35 ilizokuwa imebeba, lilitolewa na kampuni ya Bw Allen ya Vulcan siku ya Jumapili

Nyambizi ya Ujerumani iliyozama wakati wa vita vya kwanza vya dunia yapatikana
Bomu kubwa la vita vya pili vya dunia kuharibiwa Ujerumani
Vita vya Coral Sea vinatajwa kama hatua kubwa ya kuizuia Japan kuwa na ushawishi huko Pacific wakati wa vita.

Jeshi la Marekani lilisema kuwa wanajeshi 216 waliuawa wakati meli hiyo ilishambuliwa. Zaidi wa wengine 2,000 waliokolewa.

Mwaka uliopita Vulcan ilingundua mabaki ya meli ya USS Indianapolis, ambayo ilizama mwezi Julai mwaka 1945.

Imegundua vyombo vingine vikiwemo meli ya vita ya Japan, Musashi na nyingine ya Italia Artigliere zote kutoka eneo hilo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad