Mpaka Kuitwa Mama si Kazi Rahisi – Linah

Mpaka kuitwa mama si kazi rahisi – Linah
Msanii wa muziki Bongo, Linah amecharukia vikali wale wanaokosoa picha za watoto wa wenzao zinapowekwa mtandaoni.

Muimbaji huyo akizungumza na kipindi cha Uhondo, E Fm amesema si vizuri kwa wenye tabia hiyo kwani hadi mtu kufikia hatua ya kuitwa mama si kazi rahisi hata kidogo.

“Mimi kama mzazi ninapoona mwenzangu ameposti picha ya mtoto wake halafu anakuja mtu anasema mtoto wake mbaya, siyo vizuri kwa sababu mpaka kuitwa mama si kazi rahisi,” amesema.

“Kwa hiyo unapokuwa unamsindika mwenzako maneno ya namna hiyo inakuwa siyo vizuri, labda huyo anayeongea hivyo hajazaa, akija kuzaa hajui itakuwaje,” ameongeza.

Soma Pia; Linah hajutii kupiga picha za utupu katika ujauzito wake

Linah alijaliwa mtoto wa kwanza July 25, 2017, kwa sasa muimbaji huyo anafanya vizuri na wimbo ‘Same Boy’ ambayo amemshirikisha Rachel ikiwa ni ngoma ya pili kufanya pamoja.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad