Mr Nice Amchana Dudu Baya "Ameyumba Kiuchumi Anasingizia Kuacha Pombe"

Mr NiceAmchana  Dudu Baya "Ameyumba Kiuchumi Anasingizia Kuacha Pombe"
Msanii muziki wa staili ya Takeu amabe anafanya vizuri kwa sasa na kibao chake kipya cha 'Tuheshimiane', Mr Nice amefunguka na kumchana Dudu Baya kuwa ameyumba kiuchumi ndio maana anasingizia kuacha pombe bila ya kusema ukweli unaomkabili.

Mr. Nice amebainisha hayo kupitia kipindi cha eNewz inayorushwa na tinga namba moja kwa vijana EATV baada ya kupita muda kidogo tokea Dudu Baya kutoa kauli yake ya kudai kwa sasa ameacha matumizi ya pombe.

"Mimi nina mpongeza kutokana sina sababu ya kumsikitia kwasababu ni maamuzi yake yeye mwenyewe, labda ameona mwili wake hauwezi kuhumudu, uchumi vitu kama hivyo. Kwa hiyo usikae kumpongeza tu muda mwingine anapaswa apewe pole maana anaweza akawa yupo katika matatizo makubwa mpaka yakamfanya akashindwa kununua hiyo pombe",amesema Mr. Nice.

Pamoja na hayo, Mr. Nice ameendelea kwa kusema "huwenda Dudu Baya ameteteleka kiuchumi ndio maana anasingizia kuacha pombe lakini mimi naendelea na maisha yangu, kuburudika ni moja ya sehemu ya maisha yangu maana wote hatuwezi tukafanana".
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad