Mtaalamu wa Nyoka Alivyouawa na Cobra


Upo msemo unaosema ‘Mganga hajigangi’ na ndio msemo unaoweza kuutumia kwenye tukio moja lililomkuta mwanaume mmoja ambae ni raia wa Malaysia ni maarufu kwa jina la ‘mwanaume anayemudu’ nyoka.

Mwanaume mmoja ajulikanaye kwa jina la Abu Zarin Hussin ambaye taaluma yake alikuwa ni Askari wa Zimamoto akiwa amepitia mafunzo maalumu ya kukabiliana au kuwamudu nyoka, ameripotiwa kufa siku za hivi karibuni kwa kung’atwa na nyoka.

Mtaalamu huyo wa nyoka anadaiwa kung’atwa na nyoka aina ya cobra hadi kupoteza maisha akiwa katika shughuli zake za kila siku, Jumatatu ya March 12, 2018 na kupelekwa hospitali kwa matibabu, lakini akafariki mnamo March 16, 2018.


Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad