Mzee Akilimali Amuwakia Mkwasa "Acha Kuudanganya Umma"

Mzee Akilimali  Amuwakia Mkwasa "Acha Kuudanganya Umma"
Katibu wa Baraza la Wazee wa Yanga, Ibrahim Akilimali, amemuomba Katibu Mkuu wa klabu hiyo kuacha kuudanganya umma.

Kauli ya mzee Akilimali imekuja mara baada ya kikosi cha leo kitakachocheza dhidi ya Township Rollers FC kuwekwa wazi huku baadhi ya wachezaji waliotajwa kuwepo wakikosekana.

Katika mkutano alioitisha jana na waandishi wa habari, Katibu Charles Mkwasa, alisema wachezaji Thaban Kamusoko, Yohana Nkomola pamoja na Ramadhan Shaibu 'Ninja' watakuwa fiti asilimia 100 kucheza leo.

Akilimali amemuomba Mkwasa kuwa mkweli haswa linapotokea suala la mechi za kimataifa, kwani huhitaji kikosi chenye wigo mpana na si kuwadanganya watu kuwa fulani atakuwepo kisha baadaye akosekane.

Na kuelekea mchezo wa leo, Akilimali amewaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi kuipa hamasa timu yao, ili iweze kusonga mbele katika Ligi ya Mabingwa Afrika.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad