Rufaa ya Kupinga Hukumu ya Kifungo ya Sugu, Masonga Yapelekwa Mahakama Kuu

Rufaa ya Kupinga Hukumu ya Kifungo ya Sugu, Masonga Yapelekwa Mahakama Kuu
Rufaa ya kupinga hukumu ya kifungo cha mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga wanaotumikia jela miezi mitano imewasilisha Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya jana Machi 1, 2018 na mmoja wa mawakili wa Sugu, Faraji Mangula na kupewa kumbukumbu namba 29/2018.

“Tayari rufaa yetu imepokelewa katika Mahakama Kuu (Mbeya), sasa tunasubiri ni kupangiwa tarehe ya kuanza kusikiliza. Tunawashukuru watu wa Mahakama hii wameshughulikia vizuri jambo hili,” alisema Mangula.

Mawakili hao wamekusudia kuomba dhamana kwa Sugu na Masonga ili wawe kuwa nje katika kipindi ambacho watakuwa wanasikiliza rufaa yao.

Sugu na Masonga walihukumiwa baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli ambapo walitoa kauli hiyo Desemba 30, 2018 katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad