Uzuri Wangu Huwa Mademu Wakati Wote Wamenizunguka- Prezzo

Uzuri Wangu Huwa Mademu Wakati Wote Wamenizunguka- Prezzo
Rapper kutoka nchini Kenya, Prezzo amejibu kuhusu tetesi za kuchana na aliyekuwa mpenzi wake Amber Lulu.

Prezzo ambaye kwa sasa yupo Tanzania kwa ajili ya promotion ya ngoma yake na Dogo Janja ameiambia FNL ya EATV kuwa kuachana kwao ni baada ya Amber Lulu kumuona na wanawake wengine bila kujua ukweli wa ukaribu wao ila bado anampenda.

“Uzuri wangu mimi huwa na mademu wakati wote wamenizunguka, shida nyingine mtu akiniona na demu fulani labda ni dada au binamu yangu kwa sababu mimi nina familia Tanzania tayari ni kosa,” amesema Prezzo.

Licha ya kauli hiyo ya Prezzo bado wawili hao wameonekena wakiwa pamoja kwenye mitandao ya kijamii, siku ya jana Amber Lulu katika ukurasa wake wa Instagram alipost picha wakiwa pamoja na kuandika; ‘Napenda nnyaa kama Mende ilo tendo tulitendee #hamsamia’.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad