Wambura Jembe Lisilokubali Kushindwa Katika Soka, Aamua Kukata Rufaa Akiwa na Hizi Sababu Tano Mkononi

Wakili anaemtetea Michael Wambura, Emanuel Muga amesema kwamba, wao wameamua kukata rufaa ili kutafuta haki ya mteja wake.

Muga amesema katika rufaa hiyo imesheheni masuala ya kisheria na kuna sababu tano za msingi zilizowafanya waamue kupeleka rufaa mbele ya kamati ya maadili ya rufaa.

“Kinachofuata ni hatua ya rufaa, tumeshaandaa rufaa na ipo tayari tumeshailipia kwa mujibu wa kanuni lazima ilipiwe silingi milioni moja (1,000,000) na tumeanza utaratibu wa kuisajili pale TFF ndani ya siku tatu ambazo zimetolewa.

“Rufaa imesheheni masuala ya kisheria, ina sababu tano za msingi na tutakuwa tayari kwenda mbele ya kamati ya rufaa ya maadili ili tuweze kuzifafanua hizo sababu tano.

Hukumu kutoka kamati ya maadili mmeshaipata?

“Hukumu tumeipata ikiwa imechapwa lakini kwenye tovuti na tuliisikiliza lakini kanuni hazisemi kwamba tuiambatanishe wakati kunakata rufaa kwa hiyo tumeamua kukata rufaa ingawa haijatufikia rasmi kwa sababu tumekata rufaa kwa hati ya dhalura kwamba kamati ya rufaa ya maadili iitwe haraka kwa hati ya dharura ili isikilize hili suala itolee maamuzi ili mambo mengine yaendelee.
“Wambura hawei akabaki amefungiwa tu ni mtu ambaye anamajukumu mengi ya kitaifa na kimataifa, ikumbukwe kwamba aliteuliwa kuwa mechi kamishna wa mechi itakayochezwa mwezi ujao ya U20 kati ya Kenya na Rwanda kwa hiyo hatima yake lazima ijulikane kabla ya mwezi Aprili ili aweze kufanya hayo majukumu.
“Kwa hiyo tunaiomba TFF kwa hati ya dharura iitwe hiyo kamati ya rufaa ya maadili ili iweze kusikiliza na hatma ijulikane.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad