Watetezi wa Haki za Binadamu Waitaka UDSM Kumfutia Adhabu Abdul Nondo " Wasipofanya HivyoTutawafikisha Mahakamani"

Watetezi wa Haki za Binadamu Waitaka UDSM Kumfutia Adhabu Abdul Nondo " Wasipofanya HivyoTutawafikisha Mahakamani"
Taasisi ya watetezi wa haki za binadamu Tanzania, THRDC imeuomba uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) kumrudisha mara moja masomoni Mwanafunzi wa chuo hicho ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi nchini (TSNP) kwani kupata elimu ni haki yake ya msingi.


Mratibu wa THRDC, Onesmo Olengurumwa amesema kuwa wataandika barua ya kuuomba uongozi wa UDSM kufuta adhabu waliyompa Abdul Nondo ya kusimamishwa masomo kwa hadi kesi yake itakapomalizika na endapo watashindwa kufanya hivyo basi, THRDC watachukua hatua za kuufikisha uongozi huo mahakamani kudai haki zaidi.

Juzi Machi 26, 2018 Uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ulitoa taarifa ya kumsimamisha masomo, Abdul Nondo hadi kesi mbili zinazomkabili mkoani Iringa za kutoa taarifa za uongo mtandaoni na kudanganya kutekwa zitakapomalizika.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad