Aveva Afika Mahakamani Akiwa na Hali Mbaya Atembea Akishikiliwa

Aveva Afika Mahakamani Akiwa na Hali Mbaya Atembea Akishikiliwa
Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva ambaye alikuwa akiugua kwa muda mrefu, leo Aprili 5, amefika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuhudhuria kesi yake inayomkabili licha ya hali yake kuonekana imedhoofika huku akishikwa mkono kumsaidia kutembea.



Akiwa mahakamani hapo, muda mwingi alionekana kusaidiwa na makamu wake Godfrey Nyange maarufu kama Kaburu ambaye ni mtuhumiwa mwenzake katika kesi hiyo ambapo wawili hao wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, nyaraka na kutakatisha fedha kiasi cha Dola za Marekani 300,000.



Katika kesi hiyo, upande wa mashtaka umeiomba mahakama kusogezwa mbele kesi ili kubadili hati ya mashtaka na kuongezwa mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo. Aidha, mahakama imeahirisha kesi hadi April 12, mwaka huu.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad