Baada ya P-Square na Diamond, Rick Ross kuwaibukia Sauti Sol

Wakati leo April 28, 2018 msanii kutoka nchini Marekani, Rick Ross akitarajiwa kufanya show nchini Kenya, rapper huyo ana mpango wa kuacha alama katika nchi hiyo.

Akizungumza na NRG Radio Rick Ross amefunguka kuhusu mipango ya kufanya kolabo na kundi la muziki kutoka nchini Kenya, Sauti Sol.

Endapo kolabo hiyo itafanikiwa kutoka Sauti Sol watakuwa wasanii wa watatu Afrika kufanya kolabo na Rick Ross mara baada ya kundi la P Square kutoka Nigeria ambao mwaka 2012 walitoa wimbo uitwao Beautiful Onyinye, mwaka 2017 Diamond alimshirikisha rapper huyo katika ngoma yake ‘Waka’.
Tags

Top Post Ad

Below Post Ad