Basata 'Nandy Anahitaji Kupewa Moyo Kwa Kuwa Tukio Hilo Limemuumiza'

Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), Godfrey Mngereza amesema mwanamuziki Nandy ambaye picha zake za utupu zilivuja anahitaji kupewa moyo kwa kuwa tukio hilo limemuumiza.

Akizungumza na MCL Digital leo, amesema jamii iache kumlaumu mwanamuziki huyo, kwani kilichompata kinaweza kumtokea yeyote hasa katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia.

Amesema kama Baraza wamemuita na kuongea naye kwa ajili ya kumpa moyo na kueleza hayupo katika hali nzuri kwa sasa na anahitaji kupatiwa ushauri wa kisaikolojia.


Chanzo: Mwananchi

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad