Mchungaji Lwakatare: Mwisho wa matatizo umekaribia

Waumini wa Kanisa la Mikocheni B Assemblies of God jijini Dar es Salaam leo wameadhimisha Sikukuu ya Pasaka ambayo ni kumbukumbu ya kufufuka kwa Mkombozi wao Yesu Kristo, huku wakiondoka na ujumbe wa amani na matumaini katika maisha yao.

Katika mahubiri na salamu zake za Pasaka, Mchungaji Kiongozi Dkt Getrude Lwakatare amewasihi watanzania kupendana na kudumisha amani, huku wakiamini kuwa kifo na hatimaye kufufuka kwa Yesu Kristo, ni ishara tosha kwamba mwisho wa matatizo yanayomkabili kila mtu katika maisha yake umekaribia.

Akifafanua salamu zake hizo, Dkt Lwakatare amesema kama ilivyotokea kwa Yesu Kristo, watanzania na hususani waumini wa dini ya Kikristo wanapaswa kuwa na imani kuwa matatizo pamoja na shida mbali mbali zinazowakabili mwisho wake umekaribia.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad