Msimamo wa Rais Magufuli Kuhusu Serikali Kugawa Ng'ombe Longido


"Nimewaita Wabunge wa Arusha hapa waje waeleze shida zao. Shida hizo nimezipokea, lakini ni shida moja tu nataka niijibu hapa, ile ya kugawa ng'ombe. Sigawi Ng'ombe Mimi

Ninafahamu Mzee wangu Kikwete alienda kuwagawia ng'ombe kule Longido. Hilo Mimi siliwezi!

Tukianza na utaratibu huu; Ng'ombe wanakufa halafu Serikali inagawa, Pamba zikikauka Serikali inagawa, Korosho zikiharibika Serikali inagawa, hilo Mimi siliwezi nataka nizungumze wazi

Kwahiyo sitopeleka Ng'ombe Longido nataka niwaeleze hivyo. Zilizogawiwa wakati ule ni hizo hizo. Sijawahi kuahidi kugawa ng'ombe. Huyo ndio Magufuli!"
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad