Mwanaume Aliyezaa na Masogange Afunguka Mambo Mazito

Mwanaume Aliyezaa na Masogange Afunguka Mambo Mazito
SIKU moja baada ya mazishi ya aliyekuwa mwigizaji wa filamu na video queen maarufu Bongo, Agness Gerald Waya ‘Masogange’ yaliyofanyika juzi, jioni, kijijini kwao, Utengule-Usongwe wilayani Mbalizi jijini Mbeya, mwanaume aliyezaa naye, Sabri Shaban, kwa mara ya kwanza amezungumza na Risasi Mchanganyiko na kuelezea mapya kuhusu maisha yake na staa huyo.



MTOTO MIAKA 11

Kabla ya msiba huo, Sabri aliyezaa na Masogange mtoto mmoja wa kike aitwaye Sanie Sabri mwenye umri wa miaka 11, hakuwa akifahamika kwa watu wengi. Pia watu wengi walikuwa wakishindwa kujua kama Masogange ana mtoto au la.



WASHIRIKIANA MALEZI

Katika mahojiano maalum na gazeti hili, baada ya msiba huo mzito, Sabri alisema kuwa, kifo cha Masogange kimeacha pengo kubwa mno katika maisha yake kwani walikuwa wakishirikiana katika malezi ya binti yao huyo ambaye kwa sasa yupo darasa la saba.



KILA MMOJA NA MAISHA YAKE LAKINI…

Alisema kwamba, licha ya kuwa alikuwa yeye na Masogange hawakuwa pamoja kwa miaka mingi iliyopita huku kila mtu akiwa na maisha yake baada ya kumzaa mtoto huyo, bado walikuwa wanampa malezi mazuri mtoto huyo kwani kuna wakati alikuwa akiondoka kwa baba yake (Sabri), Magomeni na kwenda kuishi kwa mama yake (Masogange), Makongo- Juu jijini Dar kisha kurejea tena kwa baba yake.

“Ni pigo kubwa sana kwangu na kwa mwanangu Sanie. Alikuwa ametuzoea mimi na mama yake. Tulikuwa tunamlea mtoto wetu pamoja. Hata yeye (Sanie) alifurahia sana uwepo wa mama yake.



AENDA KUMPUMZISHA MZAZI MWENZAKE

“Sasa tunaongea hapa, mama yake hayupo tena. Kwa kweli Agness (Masogange) ameniachia pengo kubwa sana maishani mwangu, ninamuomba Mungu ampe nguvu mwanangu (Sanie) katika kipindi hiki kigumu,” alisema Sabri ambaye alisafiri na msiba hadi Utengule, Mbalizi jijini Mbeya kushuhudia mzazi mwenzake akipumzishwa kwenye nyumba yake ya milele.

Top Post Ad

Below Post Ad