Pete ya Uchumba Yamtoa Bonge la Povu TID "Usipende Kufuatilia Mapenzi ya Watu"

Povu la TID Baada ya Kuulizwa Kuhusu Mpenzi Wake Aliyemvalisha Pete ya Uchumba 2010 "Usipende Kufuatilia Mapenzi ya Watu"
Msanii wa muziki Bongo, TID amekata kuzungumzia lilipofia penzi lake na mrembo aliyemvisha pete ya uchumba mwaka 2010.

Muimbaji huyu anayetamba na ngoma ‘Wewe Dada’ katika mahojiano na E-Newz ya EATV alisema hapendi kuzungumzia mambo ambayo tayari yameshapita.

“Hiyo sasa it’s very long time, i am not here to discus about my past, you should know that, usipenda kufuatilia mapenzi ya watu hilo ndio tatizo lako,” amesema TID.

Katika hatua nyingine TID amekanusha taarifa zilizodai kuwa anaoa Juny mwaka huu kwa kusema sasa hivi watu wanataka kutengenezea kiki kwa kitendo cha kuoa, kwa hiyo yeye sio mtu kutafuta kiki kwa kutumia ndoa.

Top Post Ad

Below Post Ad