Ijumaa Mahakama ilimhukumu kwa mashtaka ya ufisadi, lakini alikimbilia katika makao makuu ya muungano wa wafanyakazi mjini Sao Paolo, ambako wafuasi wake walitaka asijisalimishe.
Televisheni nyingi nchini Brazil zimeonesha alivyowasili kwa helikopta katika Makao Makuu ya Polisi katika mji wa Curibita.
Lula alitoa hotuba katika mji wa Sao Bernardo do Campo kabla ya kujisalimisha, Lula amejitaja kuwa raia aliyekasirishwa na mashtaka ya kutungwa ya ufisadi.