“Sijafurahishwa na ushindi wa goli moja” Mgosi alitaka Yanga wafungwe ngapi?

Wanasema ushindi ni ushindi haijalihi ni wa aina gani lakini legendary wa Simba Mussa Hassan Mgosi kwa upande wake anasema hajafurahia Simba kupata ushindi mwembamba wa goli 1-0 dhidi ya Yanga.

Mgosi ambaye amewahi kuitumikia Simba kwa nyakati tofauti kama mchezaji na baadae akiwa meneja anasema, ni jambo jema Simba imepata pointi tatu lakini anaamini timu yake ilikuwa na uwezo wa kufunga goli zaidi ya moja.

“Yanga walitakiwa wapigwe goli sita na kuendea kwa sababu walikuja kutafuta sare wakawa wanaupoza mchezo lakini Simba wangecheza kwa speed yao ileile tulikuwa tunawafunga nyingi”-Mussa Mgosi.
Tags

Top Post Ad

Below Post Ad