Simba Yasubiri Point Tano Kuwapokonya Yanga Ubingwa VPL

Simba Yasubiri Point Tano Kuwapokonya Yanga  Ubingwa VPL
Ushindi wa Simba wa goli 1-0 dhidi ya Yanga unaifanya Simba ambayo imecheza michezo 26 ya Ligi na kusaliwa na michezo minne, ili iwe Bingwa bila ya kujali matokeo ya timu nyingine Simba inahitaji point tano yaani ishinde mchezo mmoja na itoke sare mchezo mmoja.

Kwa upande wa Yanga wao ili kutetea Ubingwa wao kunategemeana na Simba apoteze mechi tatu huku yeye akipata matokeo chanya, baada ya ushindi huo kocha wa Simba Pierre Lechantre amewaambiwa wachezaji wake kuwa sasa wanahitaji ushindi game moja na sare moja.

Tags

Top Post Ad

Below Post Ad