
Hayo yamebainishwa na taarifa zilizotolewa na mamlaka hiyo jioni ya leo (Ijumaa) na kudai kutakuwepo vipindi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 katika saa 24 ambavyo vinatarajiwa katika maeneo ya mkoa wa Tanga, Dar es Salaam, Morogoro, Lindi, Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.
Aidha, TMA imewashauri wakazi wa maeneo yaliyotajwa kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa pamoja na tahadhari zinazotolewa.
