Alikiba mwambie Diamond apatane kwanza na Baba yake ndio arudi kwako, Diamond ni mswahili na Mnafiki usimuamini

Mdau Kaamua Kufunguka:


Alikiba mimi kama shabiki yako naomba usimamie msimamo wako uleule usikubali kuyumbishwa na mtu mnafki kama Diamond, ambaye amekuwa akikupiga vijembe mara kwa mara huku akiigiza kuwa anataka kupatana na wewe na muwe kitu kimoja

Mwambie akapatane kwanza na baba yake mzazi ambaye anamchukia ndio arudi kwako, haiwezekani mtu ashindwe kumsamehe au kupatana na mzazi wake aliyemtoa kiunoni alafu aje kwako mtu baki tu ajifanye kuwa anataka mpatane

Hata kumpa mkono skuile ya msiba ulijishusha sana ,kwani ilibidi Diamond aanze kwanza kumpa mkono baba yake mzazi ndio aje kwako yule mtu ni mnafiki nakushauri kuwa nae makini

By Mtotomtamuu

Top Post Ad

Below Post Ad