Baada ya Kutandikwa Bao Nne Yanga Kurejea Dar Leo

Baada ya Kutandikwa Bao Nne Yanga Kurejea Dar Leo
Baada ya kupoteza mchezo wa jana ukiwa ni wa kwanza katika hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika, kikosi cha Yanga kinatarajia kuanza safari ya kurejea nchini leo.

Yanga ilikubali kuanza vibaya dhidi ya USM Alger kwa kufungwa idadi ya mabao 4-0, mechi ikipigwa majira ya saa 4 usiku wa jana.

Yanga itaanza safari yake kwa kupitia nchini Dubai kisha kuanza tena safari ya kuendelea kurejea Tanzania.

Matokeo hayo ni mwanzo mbaya kwa Yana kutokana na kipigo hicho kikali ambapo sasa inahitaji kuweka nguvu nyingi katika michezo mingine itakayofuata kwenye kundi hilo.

Ukiachana na USM Alger, ikumbukwe Yanga ipo na timu za Rayon Sports ya Rwanda na Gor Mahia FC ya Kenya.
Tags

Top Post Ad

Below Post Ad