Baada ya Liverpool Kuchezea Kichapo Kipa Wake Atishiwa Maisha

Baada ya Liverpool Kuchezea Kichapo Kipa Wake Atishiwa Maisha
Polisi wa eneo la Merseyside, Uingereza wamesema wanafahamu kuhusu vitisho vya maisha ambavyo vimetolewa dhidi ya mlinda lango wa Liverpool Loris Karius baada ya kuchezwa kwa fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Jumamosi.


Maafisa wamesema vitisho vyovyote vinavyotolewa kupitia mitandao ya kijamii vinafaa kuchunguzwa kwani ni hatari kwa usalama kwa usalama kwani mashabiki wanamihemko na hasira ya kukosa ubingwa.

Karius, 24, na familia yake wamekuwa wakipokea vitisho baada ya makosa mawili kutoka kwake kuwasaidia Real Madrid kupata ushindi wa 3-1.

"Tunachukulia ujumbe huu wa vitisho kwenye mitandao ya kijamii kwa uzito sana. Visa hivi vitachunguzwa," polisi wamesema.

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp, ambaye bado hajashinda kikombe tangu ajiunge na Liverpool 2015 amesema anamuonea huruma sana karius.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad