Diamond Aingia Location na Miri Ben-Ari UK Kutengeneza Video ya Baila

Diamond Aingia Location na Miri Ben-Ari UK Kutengeneza Video ya Baila
Safari ya Diamond nchini Uingereza haijakuwa kwaajili ya kufanya show bali ameitumia kuteneneza video ya wimbo wake wa Baila ambapo mrembo Miri Ben-Ari amesikika akilicharaza vizuri Violini.

Diamond ameonekana kwenye baadhi ya picha na video akiwa location nchini humo akitengeneza video hiyo ambapo inaweza ikawa ndio kichupa kinachofuata baada ya African Beauty.

Lakini kubwa zaidi Miri Ben-Ari na yeye ameonekana location baada ya kusafiri kutoka mjini New York, Marekani mpaka London ambapo inadaiwa ndio video hiyo inatengenezwa.



Tags

Top Post Ad

Below Post Ad