Kisiwa Kikubwa cha Hawaii Kimepigwa na Kimbunga Kikali na Volkano

Kisiwa Kikubwa cha Hawaii Kimepigwa na Kimbunga Kikali na Volcano
Kisiwa kikubwa cha Hawaii kimepigwa na kimbunga kinachotajwa kuwa kikali taangu mwaka 1975.

Kimbunga hicho cha kipimo cha ritcha 6.8 kimewafanya watu kuondoka majumbani mwao, pia kikiharibu miundombinu ya umeme na maji.

Kimbunga hicho kinatajwa kuanzia kwenye mlima wa volcano uitwao Kilauea. Kwa mujibu wa mashuhuda, tetemeko hilo liliambatana na upepo mkali ambao uliharibu vitu mbalimbali.

Mamia ya wakaazi wa eneo hilo tayari wametafuta hifadhi kutoka maeoe ambayo hayajaathirika.

Maija Stenback, shuhuda wa kimbunga hicho

Tunaishi eneo la mashambani Leilani, karibu vitalu sita vilisambaratishiwa mbali na mlipuko.tuliondolewa eneo hilo saa kadhaa zilizopita na sasa tumejihifadhi kwa marafikiu.

Nusu saa baada ya kimbunga hicho , nilishangaa kukuta mitandao mingi imeandika juu ya tukio hilo , kwa hiyo mimi na binti yangu tukatoka kwenda kujionea kwa macho yetu kwakweli unaweza kusikia na kuhisi mlipuko ukiwa umbali wa nusu maili na kadiri unavyokaribia eneo la tukio ndivyo unavyozidi kulihisi .Ilikuwa kama wakati mtu anavyopiga gitaa la besi kwakweli nzito, na unaweza kuhisi kweli nguvu ya uji wa volkano, rangi nayo sasa ilikuwa ya kustaajabisha na sauti ya volkano hiyo kwakweli ni maajabu makubwa .
Tags

Top Post Ad

Below Post Ad