Kuna Tofauti Kubwa ya Uchekeshaji na Ufanyaji Ujinga, Mdau Amchana Live Idriss Sultan Adai ni Mfanyaji Ujinga


Mdau mmoja Kutoka JF Ameamua Kumtolea uvivu Mchekeshaji Idriss Sultan na Kudai sio mchekeshaji, Jisomee Mwenyewe Mdau Alivyofunguka:

"Ninaomba ieleweke wazi sina bifu na Idris Sultan wala sijawahi kuwa na bifu naye ,ila penye ukweli lazima pasemwe huyu bwana mdogo ni mfanya ujinga na mambo ya kitoto toto ambayo yeye binafsi anadhani anatuchekesha kumbe tunamuona ni punguani tu asiye jielewa.

Mbali na yeye wengine wanaomfuatia kwa kufanya ujinga huku wakidhani wanatuchekesha ni Mkali wao na Dullvani wote hawa ni wafanya ujinga na mambo ya kipuuzi puuzi yasiyoeleweka.

Kwa ambao mpo karibu na Idris Sultan mwambieni tumechoka kuona mambo yake ya kipuuzi abadilike anatuboa " By Hance Mtanashati

 SOMA Pia: Job Opportunity at Workforce Management and Consultancy, Marketing Executive

Top Post Ad

Below Post Ad