Kuzuiwa Meli ya Mafuta ya Kupikia Bandarini..Viwanda Vikubwa Vinne vyasitisha Uzalishaji, Wafanyakazi 4000 Kuathirika


DAR: Viwanda vinne vikubwa vya kuzalisha mafuta ya kula vinadaiwa kusitisha uzalishaji kwa takribani mwezi mmoja sasa baada ya kuzuiwa kwa meli mbili zenye mafuta ghafi katika bandari ya dar

Mwenyekiti wa Chama cha Watengeneaji mafuta ya kupikia Tanzania, Hussein Kamote amesema viwanda hivyo vinatengeneza mafuta ya kula ya kutokana na mchikichi na kukidhi mahitaji ya zaidi ya 80% ya watanzania

Amesema mafuta hayo yanayoagizwa kutoka Indonesia na Malaysia yapo bandarini mpaka sasa kwa kuwa TRA imekataa kuyatoa

Aidha amesema kusitishwa kwa uzalishaji kumeathiri zaidi ya wafanya kazi 4000 ambao kwa sasa inabidi wasiende kazini kwa kuwa hakuna uzalishaji
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad