Nape Nnauye Bado Amlilia Marehemu Bilago Atoa Ujumbe Mzito

Nape Nnauye Bado Amlilia Marehemu Bilago Atoa Ujumbe Mzito
Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye anamkuru Mungu kwaajili ya Mbunge wa Jimbo la Buyungu, Mh. Kasuku Bilago aliyefariki Mei 26, 2018 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.

Nape amesema tangu wakutane naye kwa mara ya kwanza Bungeni amejifunza mengi kutoka kwa mbunge huyo na pengo lake ni kubwa halielezeki.

“Kaka na rafikiangu Mwl. Bilago umetangulia mbele ya haki. Ninamshukuru Mungu kwa maisha yako, toka tulipokutana Kwa Mara ya kwanza Bungeni nimejifunza mengi toka kwako, hakika pengo lako ni kubwa sana halielezeki. Umeacha alama katika siasa za nchi yetu!,” ameandika Nape katika mtandao wake Twitter.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad