Ommy Dimpozi Amuumbua Shabiki Aliyemwambia Hajui Kuimba

Ommy Dimpozi Amuumbua Shabiki Aliyemwambia Hajui Kuimba
Siku ya May 1,2018 staa wa Bongo Fleva Ommy Dimpoz aliachia ngoma yake ya “Yanje” aliyomshirikisha Seyi Shay kutokea Nigeria na baadhi ya mashabiki walikuwa wakitoa mrejesho kuhusiana na ngoma hiyo ya Yanje.

Kupitia instagram account ya Ommy Dimpoz ameonekana kumjibu shabiki ambaye hajaikubali ngoma hiyo kuwa ni hit na inapendwa na watu wengi kutokana tu na feedbacks za watu ambao wengine wameonekana kuikubali ngoma hiyo na wengine kuikataa.

Shabiki alicomment kwa kuandika “Bola uludi Kigoma tu, hujuhi kuimba” baada ya comment hiyo Ommy Dimpoz akamjibu kwa kuandika “bora mimi sijui kuimba kuliko wewe usiejua Kiswahili BOLA(BORA) ULUDI(URUDI) HUJUHI(HUJUI)”

Top Post Ad

Below Post Ad