Rais JPM Awapa Onyo Kali Wanachuo wa SUA "Sitosita Kuwafukuza Wote''

Rais JPM Awapa Onyo Kali Wanachuo wa SUA "Sitosita Kuwafukuza Wote''
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amesema hatosita kufukuza wanafunzi wa chuo watakaobainika kufanya vurugu shuleni na kuacha kuzingatia masomo, na suala hilo sio vitisho bali ni ukweli mtupu.


Rais Magufuli ameyasema hayo leo alipokuwa kwenye ziara yake Chuo Kikuu cha Kilimo cha SOkoine (SUA) mkoani Morogoro, na kuwataka wanafunzi wote vyuoni kuzingatia masomo yao, na sio kujihusisha na vurugu hasa za kisiasa, kwani akigundua hilo atafukuza wote hata kama ni chuo kizima, na iwapo atafanya hivyo, hajui kama atawarudisha tena chuoni.

"Niwaombe ndugu zangu, mmekuja hapa kwa ajili ya shule, msipoteze muda wenu kwenye masuala yasiyo na tija, tumieni muda wenu kwenye masuala ya shule, msigeuze vyuo kuwa sehemu za siasa, siasa mtazikuta tu, pigeni shule msiingie kwenye mikumbo, kila moja ana maisha yake na baba yake na mama yake, someni, pasua, kazingatieni hilo, nataka niwaeleze kiukweli, kama kutatokea chuo chochote kinafanya fujo, mimi wala sitasita kufukuza, na nikifukuza sifahamu ntawarudisha lini, hili siwatishi nawaeleza ukweli", amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ameendelea kwa kusema kwamba serikali kupitia wizara ya elimu itahakikisha inkilinda chuo cha Sokoine kama mboni ya jicho, kutokana na upekee ulionacho chuo hiko.

Tags

Top Post Ad

Below Post Ad