Bei ya Picha za Wizkid Katika Maonyesho ya D&G ni Kufuru

Bei ya picha za Wizkid katika maonyesho ya D&G ni kufuru
Baada ya staa maarufu kutokea Nigeria Wizkid “Starboy” kupata nafasi ya kufanya maonyesho ya nguo za mwanamitindo maarufu duniani Dolce & Gabanna siku ya June 15,2018 Milan,Italy.

Unaambiwa picha za staa huyo zilizopigwa katika maonyesho hayo zinauzwa  zaidi ya Shilingi laki saba mpaka Milioni moja za kitanzania hii ni baada ya kampuni moja inayojihusisha na picha kuingiza picha hizo katika mtandao wa Getty Images na kuuzwa pound 340.



Katika maonyesho hayo yaliyofanyika siku chache zilizopita Wizkid alikuwa pamoja na mwanamitindo mkongwe kutokea Marekani Naomi Campbell pamoja na Tinnie Tempah na wanamitindo wengine.

Top Post Ad

Below Post Ad