CCM Itafutika Kusini, Huku Nikutudharau - Nape Nnauye

CCM itafutika Kusini, huku nikutudharau - Nape Nnauye
Mbunge wa Jimbo la Mtama (CCM) Nape Nnauye, akichangia hoja katika mjadala wa kupitisha Bajeti Kuu ya serikali 2018 / 2019 iliyowasilishwa Bungeni na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt Philip Mpango amesema,


"Nilipoleta hoja hapa ilikuwa ni hoja ya kusimamia utekelezaji wa sheria, sheria haisimamiwi, tunakumbusha isimamiwe hela ziletwe, Badala ya kutuletea hela zetu Dk. Mpango unaleta sheria ya kuzifuta kabisa asilimia mia zije kwenu, kwa kweli huku nikutudharau kwa hali ya juu, hii si sawa, zungumzeni namna ya kuleta hela mlizochukua hii habari ya sheria mnayotaka kubadilisha toeni kwanza." Nnauye Amesema


Vile vile ameongelea swala la kusemekana kuwa na matumizi mabaya ya fedha kwenye mfuko wa zao la korosho, na kuuliza swali kuwa dawa ya kutibu tatizo hilo je nikuufuta mfuko huo, au kuchukua hela? ambapo alishindwa kujizuia kwa uchungu na kuongelea kuwapo kwa hati chafu za Hazina, na kumtaka Waziri wa fedha Dk. Mpango kuwa na huruma ambapo kama hawatakuwa makini CCM itakufa Kusini mwa nchi, Hivyo amemtaka Dk. Mpango kurejesha pesa zao na kubadilisha uamuzi ambao wameuchukua.

Top Post Ad

Below Post Ad