Diamond Akalia Kuti Kavu Kwa Zari, Mtangazaji Maulid Kitenge Ajipanga Kupeleka Posa Kwa Zari

Wakati mwanamuziki Diamond Platnumz, akiendelea na harakati za kumrudisha mzazi mwenziye, Zari The Boss Lady, kundini ili waweze kurudiana na kuishi kama zamani, Mtangazaji wa kituo cha redio Maulid Kitenge amemtembelea Zari nyumbani kwake Uganda na kuwauliza mashabiki je apeleke barua ya posa?

 Kitenge amewaomba ushauri huo mashabiki zake na Watanzania kupitia ukurasa wake wa Instagram baada ya kuposti video yake na Zari wakiwa pamoja huku akimsifia kuwa ni fundi sana wa kupika na kisha kuelezea azma yake hiyo.

Top Post Ad

Below Post Ad