EU Yaongeza Ushuru kwa Bidhaa Kutoka Marekani

EU Yaongeza Ushuru kwa Bidhaa Kutoka Marekani
Jumuiya ya Ulaya EU imeanzisha ongezeko jipya la tozo kwa bidha zinazotoka Marekani kama hatua ya kulipa kisasi dhidi ya sera ya kibiashara ya Rais Trump iliyotangaza ongezeko tozo ya uingizwaji wa bidhaa za chuma na bati nchini humo.

Ongezeko hilo jipya la tozo lililotangazwa na EU linazilenga bidhaa za Marekani kama vile vinywaji vikali,Pikipiki zinzotengenezwa Marekani pamoja na maji ya matunda ya machungwa.

Ongezeko hili la tozo mpya ya EU kama hatua ya kujibu mapigo dhidi ya Marekani dhidi ya Marekani itaziathiri bidha kama tumbaku,piki piki maarufu za Harley Davidson,siagi ya karanga bidhaa ambazo kwa sasa zitakumbana na ongezeko la asilimia 25 sawa na kiasi cha yuro bilion 2.8 ambapo utekelezwaji wake unaanza rasmi leo.

Rais wa jumuiya ya Ulaya Jean-Claude Juncker amesema tozo iliyoanzishwa na Marekani dhidi ya umoja huo inakwenda kinyume na hali halisi na historia ya uhusiano uliokuwepo kibiashara kati ya EU na Marekani.
Tags

Top Post Ad

Below Post Ad